UTAFITI WA CHANJO YA VVU KUANZA MBEYA


UTAFITI wa majaribio ya chanjo ya VVU hivi katibuni unatarajia kuingia katika hatua ya mwezi huu utakao fanyika katika mikoa miwili kwa Tanzania na moja katika nchi ya Msumbiji ambao unafahamika kwa jina la TaMoVac 02 baada ya kumaliza ule wa awali.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na utafiti huo mpya wa hatua ya pili ya majalibio ya chanjo hiyo, mtafiti mkuu wa kituo cha utafitu mkoani Mbeya cha NIMR-Mbeya Dkt. Lenard Maboko amsema kuwa utafiti huo utakuwa katika majalibio ya pili ya chanjo ya VVU.

Aliitaja vituo vitatu vitakavyo husika na utafiti huo kuwa ni Mbeya, Dar es salaam kwa Tanzania na Maputo kwa Msumbiji  ambapo utaendeshwa kwa muda wa miaka miwili.

Alisema kuwa utafitu huu utachukua washiriki 80 kwa jiji la Dar es salaam washiliki 80 Mbeya na washiliki 38 kwa Maputo Msumbiji huku utafiti huu ukiwa umebuniwa kuhakikisha usalama wa mchanganyiko chanjo na kutambuaaina za witikio wa kinga zinazosisimua mwili.

Washiriki 120 Tanzania na washiriki 24 Msumbiji ambao walipatiwa mchanganyiko wa chanjo kama hizi katika utafiti wa kwanza TAMoVac 01 na kuonekana kuwa chanjo hizi zinastahimilika vizuri.

Dkt. Maboko alisema kuwa kituo cha utafiti wa magonjwa ya binadamu Mbeya  NIMR-Mbeya inafanya utafitu huo na pia utafanyika katika chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi Muhimbili, Dar es salaam pamoja na Maputo Msumbiji katika taasisi ya afya ya taifa Nchini humo.

Alisema kuwa njia hiyo imebuniwa kutoa chanjo ya VVU na imebuniwa kukinga aina mbalimbaliza virusi hivyo ambapo kutakuwa na chanjo ya msingi ya vinasaba (DNA) kipigajeki chanjo ya kirusi cha vaccinia kilichopunguzwa nguvu inachojulikana kama (MVA-CMDR) kwa pamoja zimetengenezwa kutoamchanganyiko tofautiwa antjeni za VVU za aina ya A, B, C, D na E.

Alitaja kitu kipya na cha pekee katika utafiti huo kuwa ni jinsi ambavyo moja ya chanjo hizo inavyotolewa chanjo ya vinasaba DNA ambazo zinafaida nyingi na huku wa tafiti bado wanajaribu kugundua njia njia bora ya kusitoa katika mwili wa binadamu ili ziwe na ufanisi mkubwa.