CHUNYA: WANAFUZI WAOKOTA BASTORA




 WANAFUNZI wa sule ya msingi Ifumbo ya wilayani chunya ameokota bastora wakati wakicheza mpira katika uwanja wa shule hiyo ikiwa na risasi moja.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Mbeya kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani Athumani alisema kuwa wanafuzi hao waliogota bastola hiyo inayotumia risasi za S/Gun ikiwa na risasi moja ya aina hiyo.

Alisema kuwa siraha hiyo iliokotwa na wanafuzi wa shule ya msingi Ifumbo iliyopo katika kata ya Ifumbo wilayani Chunya ambapo ilikuwa ni majira ya saa 3:00 asubuhi ambapo waliokota bastola ikiwa katika Rambo.

Athumani alisema kuwa siraha hiyo ilikuwa imeterekezwa katika pembezoni mwa kiwanja hicho cha mpira na kuhifadhiwa ndani ya mfuko wa Rambo na kuokotwa na wanafunzi hao.

Alisema kuwa kitendo cha kumiliki silaha kinyume cha sheria ni kosa la jinai na endapo mtuyeyote atakaye kamatwa atafikishwa katika vyombo vya sheria.

Pia ametoa wito kwa wananchi na hasa kwa wakazi wa wilaya ya Chunya kuwa makini na umiliki wa silaha kinyume cha sheria.