KILAMTU NI TAJILI


HAKUNA binadau aliyezaliwa kuwa fukala wala tajiri bali juhudi na uvivu ndivyo vinasababisha mtu kuwa katika hali nzuri au mbaya katika maisha.

Hayo yamebainishwa juzi jijini Mbeya na mkurugezi wa shirika la Nyumba la taifa, Nehemia Mchechu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 50 toka kuanzishwa kwa shule ya sekondari Mbeya Day ya jijini hapa.

Alisema kumekuwa na tabia ya watanzania wengi wanao jijegea mawazo kuwa wao ni maskini na mawazo yao kuwa halisi katika maisha yao.

“Watanzania wengi wanakuwa wasikini kwa kujitakia kwani wamekuwa wakijidharau na kujibweteka pasipo kujishughulisha na hatimaye kutegemea serikali iwafanyie kitu ili kujikwamua katika maisha yao,” alisema Mchechu.

Aliwataka wanafuzi wa shule huyo kuwa makini wanapojisomea na kujijengea kuwa wanataka kuwa wakina nani hapo watakapo hitimu elimu zao na hii itamfanya mwanafuzi kufikia mareko na kujiweka katika nafasi mzuri.

Alisema kumekuwa na wanafunzi wanao soma ilimradi tu katimiza wajibu wa kwenda shule na kujikuta wanahitimu kwa kupata pasi zisizo za kurizisha hii inatokana na kuto kuwa na malengo wanapo kuwa shuleni.

Katika maadhimisho hayo ya miaka 50 yaliambatana na halambee ya kuchangia ukarabati wa maabara ya shule hiyo ambayo imefanikiwa kutoa baadhi ya watu maarufu wenye nyadhifa tofauti.

Mmoja wa watu waloatoka katika shule hiyo ni pamoja na Nehemia Mchechu, Mh. Joseph Mbilinyi (Sugu) mbunge ya jimbo la Mbeya Mjini, Naibu waziri wa elimu, Philipo Mlugo hao ni baadhi tu ya watu walohitimu katika shule hiyo katika miaka yake 50.

Katika halambee hiyo shule ilifanikiwa kupata zaidi ya milioni 60 ambapo walikuwa na lengo la kupata millioni 150 kwaajili ya ukarabati wa maabara ya shule hiyo na nyumba ya mwalimu.

Mchechu alitoa wito kwa wanafunzi washule hiyo kuwa wamalizapo wakumbuke kurudi katika shule yao na kuwataka wale walio hitimu katika shule hiyo kwa miaka ya hapo nyuma kujitokeza na kujitolea kwaajili ya shule yao.