WAHITIMU KIDATO CHA NNE WAANZA KUFANYA MITIHANI YAO YA KUHITIMU



ZAIDI ya  watahiniwa  42,100 wa kidato cha nne Mkoani wameanza kufanya mtihani wao jana  huku Ofisa Elimu Mkoa wa Mbeya Bw. Juma Kaponda  akiwataka wasimamizi wa mitihani hiyo kuwa waadilifu ili kuepusha sifa mbaya ya kufutiwa matokeo  npamoja na walimu wenyewe kujishusha hadhi.

Kaponda amesema kuwa kati ya hao watahiniwa  34,159  na  wale wa kujitegemea ni 7,941 kwa mkoa mzima wa Mbeya ambao tayari wameanza mitihani jana mapema.

Akizungumza na mwandishi wa ELIMTAA ofisini kwake jana kuhusiana kuanza mtihani huo ,Kaponda amesema vituo vilivyopo vya kufanyia mtihani ni 279 na idadi ya wasimamizi ikiwa 1,323 .

Amesema kuwa mtihani huo umeanza vizuri katika maeneo yote hivyo niwaomba  wasimamizi wa mitihani hii kuwa waadilifu wazuri  tunaomba kusiwepo na udangajifu wowote katika mitihani hii ,hatutapenda tatizo hili lijirudie tena tunataka wanafunzi wetu wa Mkoa wa Mbeya wasifanye kazi ya kufutiwa matokeo .

Akizungumza tabia ya kuvuja mtihani Ofisa Elimu huyo alisema wamekugundua kuwa  tatizo la kuvuja kwa mitihani lipo kwa wasimamizi wenyewe  ambao hushindwa kuwa makini wakati wa zoezi hilo likiwa linaendelea la usimamizi wa katika vyumba vya mtihani.

Aidha Kaponda amesema kilichotokea mwaka jana cha kufutiwa matokeo kwa baadhi ya shule za sekondari Mkoani hapa kilidhalilisha sana serikali na walimu wenyewe hivyo ni muhimu walimu kulinda heshima kwani tatizo hilo linatokea sehemu ndogo sana .

Mmoja wa wananchi wa kata ya Ilomba .Atupele Musa amesema kuwa mtihani huo wa kidato cha nne umeanza vizuri hivyo ni vema kusitokee udangajifu wowote wa mtihani kama inavyokuwa siku zote.