MRADI WACHELEWA


KUCHELEWA kukamilika kwa mradi  mkubwa wa ujenzi wa  hospitali ya Wilaya ya  Mbarali Mkoani Mbeya kumesabishwa na uhaba wa Kokoto katika Kampuni ya Congolo Mswisswi  ambao ulisimama kwa muda kutokana na Tazara kugoma hivi karibuni.

Imeelezwa kuwa hospitali hiyo ilitarajiwa kukamilika mapema lakini tatizo kubwa likatokea upande wa Kokoto ambazo ililazimika kuagiza Mkoani Kibaha ambako nako walikuwa wakitumia  grama kubwa.

Akizungumza na Rock Fm ofisini kwake Mhandisi wa ujenzi wa Wilaya ya Mbarali Eng.VenatThadei Komba  kuhusiana na ujenzi huo  wa mradi wa hospitali kutokamilika mapema.

Eng. Komba amesema mradi huo kwa awamu ya kwanza unategemea kukamilika mwezi Disemba mwaka huu na kwamba awamu ya pili wameomba bajeti kwa kwaka huu na kwamba mpaka kukamilika kwake wanategemea kutumia zaidi ya bi.1.5.