SYRIA: WAASI WAPAMBANA KULIPATA ENEO LA MPAKA WA UTURUKI


Majeshi  ya  waasi  wa  Syria  pamoja  na  yale  ya  serikali yanapambana  kudhibiti  eneo  muhimu  linalodhibitiwa  na serikali  karibu  na  mpaka  na  Uturuki.

Kamanda  wa  jeshi la  waasi Abu Saeed  amesema  kuwa  waasi wanapambana  kudhibiti  eneo  la  Wadi al-Daif  katika jimbo la  Maaret al Nouman, ambako  majeshi  ya  serikali yameweka  makombora  ambayo  yanafyatuliwa  kuelekea maeneo  katika   jimbo  la  Idlib.

Mapigano  hayo  yamekuja siku  moja  baada  ya  kombora  la  Syria  kuanguka   katika jimbo  la  Hatay  nchini  Uturuki , na  kusababisha  Uturuki kulipiza  kisasi  kwa  kushambulia  kwa  makombora  ndani ya  Syria.

Shirika  la kuangalia  haki  za  binadamu  nchini Syria  limesema  idadi  ya  watu  waliouwawa  jana Jumatatu  nchini  Syria  imefikia  210  na  idadi  hiyo imefikia  watu  4,727  katika  mwezi  wa  Septemba