SERIKALI YAPONGEZA BARRICK GOLD


SERIKALI imeipongeza Kampuni ya African Barrick Gold (ABG) kwa kuleta manufaa makubwa kwa taifa kutokana na uwekezaji unaoendelea kufanywa na migodi yake nchini katika nyanja mbalimbali ikiwamo uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele, baada ya kufanya ziara ya mgodi huo uliopo Wilaya ya Tarime, mkoani Mara.

 Katika ziara hiyo, Masele pamoja na Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Charles Kitwanga, wametembelea miradi mikubwa ya jamii ambayo inatekelezwa na mgodi huo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo elimu, maji na afya.

Masele amesema mgodi wa North Mara kihistoria umekuwa na matatizo ya mahusiano na jamii inayouzunguka, lakini hatua kubwa zimepigwa sasa kuboresha mahusiano na vijiji vinavyozunguka mgodi huo.