UCHAGUZI
wa umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya umemalizika
na kupatikana vingozi wapya ambapo Aman Kajuna ameibuka kidedea baada ya
kuwamwaga wagombea wezake wawili hivyo kufanikiwa kushika nafasi ya Mwenyekiti
vijana.
Hata
hivyo uchaguzi huo ambao ulikuwa ni vitisho kwa kila mgombea ulifanyika katika
ukumbi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (MIST) kilichopo mjini hapa.
Akitangaza
matokeo hayo Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya Maganga Sengerema ambaye pia alikuwa
ni Msimamizi Mkuu wa uchaguzi huo amesema nafasi ya Mwenyekiti
imechukuliwa na Bw.Kajuna amabye amepata kura 465 akifuatiwa na
Bi.Mary Mwaijumba ameyepata kura 37 huku Bi.Lusekelo Malema akipata 35.
Amemtaja
mshindi wa nafasi ya Baraza kuu la Vijana kwa kura 393, kuwa ni Neema
Mwandabila huku wapinzani wake ambao ni Saul Mwaisenye amepata kura
184 na Richard Kayinga ameambulia kura 25.
