WAZAZI WAMETAKIWA KUWAWEZESHA WATOTO KATIKA KUBORESHA VIPAJI VYAO



WAZAZI wanatakiwa kuwa makini na waangalizi wa zuri katika kuvitambua vipaji vya watoto wao na kuviendeleza ili viwasaidie baadae katika maisha yao.

Akizungumza katika maafari ya sita ya darasa la saba yaliyo fanyika hivi karibuni katika shule ya St.Mary’s ya mkoani Mbeya na Afisa tawala wa shule hiyo, Anuciatha Ngonyani alisema kuwa wazazi wengi wamekuwa vikwazo katika kuendeleza vipaji vya watoto wao.

Alisema baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwazuia watoto wao kushiriki katika mambo mbalimbali ya kuonyesha vipaji vyao hasa katika Michezo ya aina tofauti na huku mtoto akiwa na kipaji cha kujeza na anaweza.

Ngonyani amewataka wazazi kuwa ruhusu watiti wao kushiriki katika michezo mbalimbali hasa mpira wa miguu ambapo kwa ulimwengu wa sasa ni ajira ambayo imakipato kikubwa ambacho baadhi ya marais wapo chini zaidi ya wachezaji wa mpira.

Kwa upande wa wanafunzi katika risara yao wamesema kuwa wanaomba waboreshewe viwanja vya michezo ili waonyeshe vipaji vyao walivyo navyo  na kuahidi kufanya vizuri katika mtihani wao wa darasa la saba.

Walisema wakiboreshewa viwanja hivyo vitawasaidia katika michezo mbalimbali ya hapo shuleni hapo ambayo imebainika kuna wanafunzi wengi wenye vipaji vya kimichezo.

Nae mgeni Rasmi katika maafari hayo, Haji Seliman Control wa CRDB tawi la Mbeya kwa niaba ya Meneja, alisema kuwa suala la michezo mashuleni ni muhimu sana katika kwa wanafunzi na humsaidia mtoto katika kuboresha akili yake kwani nichezo ni afya na baadae kuwa ajila yenye ujila mkubwa.

Seleman kwa kuhakikisha wanafunzi wana tumia fulsa vizuri ya kuonyesha vipaji vyao alimkabidhi afisa tawala wa shule hiyo Bi Ngonyani mipira mitatu ya kuchezwa kwa miguu na kuwataka wa wajitahidi kuwaonyesha vipaji vyao.

Alisema ombi la wanafuzi hao amelipokea na kulifikisha katika uongozi wa CRDB na kuitazama bajeti yao na huenda wataboresha viwanja vya nichezo au kuvijenga upya kulingana na bajeti yao itakavyo kuwa.

Seleman alimpa afisa tawala wa shule hiyo kazi ya kufanya tathimini ya ghalama za uboreshaji wa viwanja vivyo ili vianze kuboreshwa na kuwafanya wanafunzi kufurahia michezo na kuonyesha uwezo wao katika viwanja bora vya michezo yao.