SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA WASIO JUA KUSOMA


SERIKALI katika kukabiliana na matatizo ya kuwapitisha wanafunzi wasio jua kusoma na kuandika kuingia katika kidato cha kwanza mwaka huu waalimu wa kuu wa shule hawata ruhusiwa kusimamia mitihani badala yake kusimamiwa na msimamizi mkuu pekee.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kuwa na wanafunzi wengi wanao pasi na huku hawajui kusoma wala kuandika njia hii itasaidia kupunguza ama kuondoa kabisa suala hilo la kuwapo kwa wanafunzi wasio jua kusoma wa kuandika katika kidato cha kwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari afisa elimu wa Mkoa wa Mbeyu Juma kaponda hivi karibuni alisema kuwa ili kupambana na tatizo hilo ambalo ni changamoto kubwa kwa taifa ni vyema waalimu wakuu wakaondolewa katika usimamizi wa mitihani ya wanafunzi wao.

Suala la mwanafuzi kuingia kidato cha nne akiwa hajui kusoma wala kuandika si aibu kwa taifa bali ni changamoto kwa taifa na ibidi kukabiliana nayo.

“Suala hilo la wanafunzi kuingia katika kidato cha kwanza wakati hajui kusoma na kuandika ni si aibu kwa taifa bali ni changamoto ambayo taifa lina bidi kukabiliana nalo na katika kukabiliana changamoto hiyo waalimu wakuu hawata husika katika usimamizi wa wanafunzi wao,” alisema Kaponda.

Kaponda alisema kuwa waalimu walio simamia mikondo ambayo ilitoa wanafuzi ambao hawajuu kusoma wala kuandika wamesimamishwa katika zoezi zima la usimamizi wa mitihani ya darasa la saba kwa kipindi cha miaka mitatu.

Hatua ambayo serikali mpaka sasa imeichukua kwa sasa ni kuhakikisha inawatambua wanafuzi wote ambao mpaka wanaingia darasa la saba hawajui kusoma wala kuandika majina yao yataandikwa na wakuu wao wa shule mpaka anaingia katika chumba cha mtihani serikali itajua shule Fulani mwanafuzi A hajui kusoma wala kuandika watamuangalia mpaka wakati wa kusahisha mtihani wake wa taifa.

Hii itaisaidia serikari kujua katika halmashauri Fulani kuna wanawanafuzi kadhaa ambao hawajui kusoma wala kuandika na kama watafauru serikali itajihoji kwanini wamefauri na kama ameoteha hawawezi kuwa wengi waliootea.

Yeyote atakasesima chumba cha darasa ambacho kitatoa mwanafunzi asiyejua kusoma wala kuandika kabla hajaenda sekondari atabainika na mwalimu aliye simamia chumba hicho atachukuliwa hatua atachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha Kaponda alisema kuwa serikali kwa mwaka huu wanafunzi wa darasa la saba wata jaza majibu yao katika karatasi maalum ambalo litaiwezesha mashime kusaisha mitihani hiyo hii itasaidia kuepusha makosa madogo madogo katika usahishaji na kupunguza muda wa usahishaji wa mitihani.

Kaponda ametoa wito kwa wasimamizi wa mitihani na kusema kuwa mitihani ni vita kati ya mtahini na mtahiniwa, msimamizi akiwa anatoka nje mara kwa mara atamsababishia mwanafuzni kuingia katika vishawi vya kufanya udanganyifu.