OFISA NDANI


MKUU wa Wilaya (DC) ya Sikonge, mkoani Tabora, Hanifa Selengu, amemsweka ndani mtumishi wa halmashauri ya wilaya hiyo kwa madai ya kushindwa kuwajibika katika majukumu yake ikiwemo kutofuata maagizo yake.

Selengu amemuweka ndani Ofisa Utumishi Msaidizi wa halmashauri hiyo, Elly Arkechi kwa siku moja akimtuhumu kukwamisha kazi yake.

Tukio hilo lilitokea katika kikao cha kamati ya sherehe na maandalizi ya mbio za mwenge wa uhuru na Arkechi, amesema ni kweli alilala ndani saa 24.