TUWATA WAMWANDIKIA MKURUGENZA BARUA


MGOGORO wa ujenzi wa kituo cha wazee cha Tunaini la wazee Tanzania Tuwata limechukua sura mpya baada ya uongozi wa asasi hiyo kumuandikia mkurugezi wa jiji la Mbeya ili kupata ufafanuzi.

Akizunguza na  Rock Fm mwenyekiti wa asasi hiyo Dr. David Magogo amesema kuwa wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kumuandikia mkurugenzi wa jiji la Mbeya, Jumanne Iddy, ni kutokana na kuto rizika na barua walizo kuwa wakizipokea kutoka katika ofisi yake.

Amesema katika barua hiyo ambayo wamemtumie moja kwa moja mkurugenzi na kuambatanisha na barua za awali ambazo waliomba kibali cha ujenzi wa kituo hicho cha huduma kwa wazee, ambazo zikiwa na mkanganyiko mkubwa wa kuruhusu na kubadilisha ombi lao la ujenzi.

Tangu julai 27 mwaka huu takribani mwezi mmoja sasa bado hawaja pokea majibu ya barua yao na kuwa Dr. Magogo na wenzake watafika katika ofisi yake kufuatilia majibu ya barua yao.