UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilayani
Monduli umekanusha madai ya Katibu wa CCM mkoani hapa, Mary Chatanda kuwa
uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali uliegemea misingi ya kundi na kusema
walipitisha majina yote kugombea.
Aidha wameeleza mpaka sasa hawajapewa taarifa rasmi juu ya
suala hilo pamoja na maelekezo yanayodaiwa kutolewa na kikao cha Halmashauri
Kuu ya chama hicho mkoa kilichokaa mwishoni mwa mwezi uliopita zaidi ya
kuzisoma kwenye vyombo vya habari.
Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Monduli, Julius Kalanga,
amesema hayo wakati akieleza mpaka sasa utekelezaji wa maagizo hayo umefikia
wapi na kueleza kushangazwa na habari hizo alizozisoma gazetini.
Amesema taarifa hizo hazina ukweli, kwani hakukuwa na kitu
kama hicho wao walipitisha majina yote ya wale waliojitokeza kugombea nafasi ya
uenyekiti wa UVCCM wilaya.
