HATUTA ANDIKA HABARI MPAKA WAHUSIKA WASHUGHULIKIWE



CHAMA cha waandishi Mkoani Mbeya kifikia azimio la kuto jishughulisha na habari za kipolisi hadi jeshi hilo litakapo wachukulia hatua wahusika wa tukio hilo na kuhakikisha kuwalinda waandishi wa habari katika matukio ya hatarishi na kutoa utatuzi kufuatia kifo cha Mwandishi wa habari wa Iringa.

Mbali ya kuandika habari zitokazo katika katika jeshi hilo waandishi wa habari wa Mkoa wa Mbeya wamepokea kwa masikitiko makubwa na kulaani kitendo kilicho fanywa na Jeshi la polisi Mkoani Iringa na kuikana tume iliyo undwa na jeshi hilo kufanya uchunguzi kuhusiana na tukiohilo.

Wana habari wamependekeza kuwa tukio hilo uchunguzi wake ufanye na watu kutoka nje ya jeshi hilo wakiwemo waandishi wa habari.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari Mwenyekiti wa Mbeya Press Club, Christopher Nyenyembe amesema kuwa  Mwili wa marehemu unatarajiwa kuzikwa katika jiji la Mbeya  wilayani Rungwe na taratibu za maziko zinafanyika huo mkoani Iringa.

Marehemu alikuwa mwandishi wa habari wa Chanel Ten, Daud Mwangosi, mkoani Iringa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo.