WAANDISHI wa habari mkoani mbeya wanatarajia kuungana na waandishi wa habari kote nchini katika maandamano makubwa ya amani kupinga mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Iringa na Mwandishi wa habari wa kituo cha Channel 10, Daud Mwangosi mnamo Sept,2 mwaka huu yaliyotokea katika Kijiji cha Nyololo mkoani humo.
Maandamano hayo yatakayowahusisha wanahabari wote mkoani Mbeya yanatarajiwa kuanzia eneo la Mafiat na kumalizikia katika kituo cha mafuta cha zamani cha Bp karibu na Ofisi za Shirika la Nyumba la Taifa(NHC),uhindini, jijini hapa.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari katika ofisi za klabu ya waandishi wa habari (MBPC),mkoani Mbeya maeneo ya uhindini jijini hapa,Katibu wa klabu hiyo, Keneth Mwazembe alisema kuwa maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika septemba,11,2012 kuanzia majira ya saa 3.00 asubuhi.
Amesema utaratibu wa kupata kibali kutoka jeshi la polisi unaendelea baada ya kupeleka maombi kwa maandishi na kuambiwa warejee saa 8 mchana kupata majibu kutokana na Mkuu wa polisi wa Wilaya kudaiwa kuwepo katika kikao.
Hata hivyo Mwazembe amesema kuwa wakati wa maamndamano hayo wanahabari wote watavaa nguo nyeusi ama kufunga kitambaa cheusi mkononi ikiwa ni ishara ya kuomboleza kifo cha mwanahabari mwenzao,wakitembea kimya bila kelele ikiwa ni njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa serikali na umma kwa ujumla.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
