WAWILI WAKAMATWA KIFO CHA MWANAFUNZI

WATU wawili wanaosadikika kuwa ni wahusika wa kifo cha binti mmoja aliyeuawa kwa kuchomwa na kisu eneo la Nzovwe Jijini Mbeya kwa kile kinachadaiwa kuwa ni kutokana na wivu wa mapenzi wamekamatwa na Jeshi la Polisi.

Habari zilizotufikia hivi Punde, zimesema kuwa wanaume hao wawili wanashikiliwa kwa mahojiano ambapo mmoja inaelezwa kuwa ndiye aliyehusika na mwingine ni anayedaiwa kuwa alikuwa na mahusiano mapya na marehemu.

Taarifa kamili kikosi kazi cha mtandao wa kalulunga kinafuatilia na baada ya kukamilisha uchunguzi kitazianika hapahapa mtandaoni.