SHIRIKISHO LA SOMALIA LASIFIWA KWA KUTIMIZA AHADI

Watetezi wa haki za binadamu wamepokea vyema mpangokazi wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia uliotiwa saini hivi karibuni wa kuacha kuandikisha askari watoto.
  • Askari wa Somalia jijini Mogadishu wanaonyesha watoto wa Somalia namna ya kutumia bunduki ya Kalashnikov. Serikali hiyo iliapa kuondoa kabisa askari watoto katika safu yake ya askari.  [Mohamed Dahir/AFP] Askari wa Somalia jijini Mogadishu wanaonyesha watoto wa Somalia namna ya kutumia bunduki ya Kalashnikov. Serikali hiyo iliapa kuondoa kabisa askari watoto katika safu yake ya askari. [Mohamed Dahir/AFP]
TFG ilitia saini mpangokazi huo tarehe 3 Julai katika mkutano wa Kikundi cha Mawasiliano cha Kimataifa kwa Somalia huko Roma, ikiapa kuchukua hatua za muhimu kuacha kuandikisha askari watoto katika jeshi la taifa. Uridhiaji kamili utasababisha kuifuta Somalia katika orodha ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ya vikundi ambavyo vinavyoajiri askari watoto, ambayo ameikuwepo tangu 2007.
Katika Mpangokazi huo, serikali ya Somalia ilikubali kuwarejesha katika jamii watoto waliotolewa jeshini na kuwaingiza asasi za kijamii kwa msaada wa Umoja wa Mataifa. Mpangokazi huo pia ulijumuisha ufanyaji wa kosa la jinai kuandikisha askari watoto katika sheria za taifa na kutoa ufikaji usiozuilika wa Umoja wa Mataifa kwenye taasisi za jeshi kuthibitisha uridhiaji huo.
Saini ya serikali kuhusu mpangokazi ni hatua ya ukaribisho mzuri, alisema Abdullahi Mohamed Hassan, mkurugenzi wa Mogadishu Media House, ambao ni amilifu katika kuhamasisha amani na kutetea haki za waandishi wa habari.
"Tunahimiza Serikali ya Mpito ya Shirikisho (TFG) kuchukua hatua muhimu kulinda watoto dhidi ya uandikishaji askari na kufanya kazi kuelekea kwenye uachiaji wa watoto wote ambao wanafanya kazi katika vikosi vya jeshi, pamoja na urekebishaji upya wa askari mtoto," aliiambia Sabahi.
"Pia tunatoa wito kwa mamlaka zinazohusika kutoa miradi ya maendeleo kuunganisha upya watoto ambao waliandikishwa askari kwa njia ya elimu, msaada wa kisaikolojia na kijamii, mafunzo ya utaalamu, na utoaji wa fursa za kazi," Hassan alisema. "Wakati huohuo, taratibu muhimu lazima zichukuliwe kuhitimisha tukio hili la kuandikisha askari watoto katika vikosi vya jeshi."
Hassan alielezea kitendo cha kuwaajiri watoto na kuwatumia kama askari kuwa ni "ukiukwaji unaosikitisha sana ambao watoto wamefanyiwa, pamoja na ukiukwaji wa sheria ya kimataifa."
"Ni uharibifu wa kimwili na kiroho kwa watoto, ndiyo maana utaratibu huu hauwezi kuvumiliwa," alisema.
Abdi Adawe Ali, mwenyekiti wa Shirika la Haki za Watoto, alisema kwamba hii ni mara ya kwanza kwa Somalia kujiunga na nchi nyingine kupambana na kuwaajiri watoto wanajeshi. "Ni muhimu sana kwamba TFG kuheshimu ahadi zao na ukosaji wa kuwaajiri watoto wanajeshi," alisema.
"Mpangokazi uliosainiwa ni hatua muhimu katika kumaliza ajira kwa wanajeshi watoto na tunatoa wito kwa serikali kutafsiri mpango huu katika taratibu zinazoshikika ambazo zinatekelezwa katika ngazi ya chini," aliiambia Sabahi.