WANANCHI WALALAMIKA

WANANCHI wa kijiji cha Shai kilichopo kata ya Mlangali wilayani Mbozi wamehuizunishwa na kitendo cha kunyang’anywa kwa ardhi ya mzee Mwamlima sababu kubwa ikiwa ni ya kisiasa.

Kwamujibu wa Afisa mtendaji wa kijiji cha Shai Bw Patrick Mkea amesema wajumbe watano ndio wanao fanya fujo na kunyang’anya mzee huyo ardhi kinyume na taratibu, hata hivyo mkutano walio ufanya wajumbe hivi karibuni ulikuwa ni kinyume cha taratibu kwa sababu hawakuwashirikisha wajumbe wa baraza la ardhi.

Hata hivyo kikao ambacho kimehudhiliwa na viongozi mbalimbali wa kata ikiwemo baraza la ardhi la kata na baraza hilo la ardhi wamedai kuwa mzee Mwamlima hana kosa bali taizo hili ni la kisiasa.

Aidha uongozi wa ardhi umetoa wito kwa tatizo la ardhi lisewa linapelekwa kwenye ofisi za kata kabla ya kupelekwa katika ofisi za baraza la ardhi kwa utatuzi.