WAMILIKI WA DALADALA WATISHIWA KUSHITAKIWA




BARAZA la Watumiaji wa Huduma za Sumatra limesema litazishtaki daladala zitakazoshiriki mgomo ulioitishiwa na Chama cha Wamiliki wa Daladala Jijini Dar es Salaam (Dacoboa).

Kauli hiyo ya baraza imekuja baada ya Dacoboa kutishia kugoma kwa madai kuwa Sumatra imekuwa ikitumia ulinzi shirikishi kuwakamata.

Katika hilo, katibu mtendaji wa baraza hilo, Oscar Kikoyo, amesema mgomo ambao umeitishwa na Dacoboa ni batili kwa sababu kulingana na kanuni za udhibiti, chama hicho hakina mkataba na wala si mtoa huduma wala hakidhibitiwi na Sumatra.