DIWANI RUNGWE: SENSA YA WATU NA MAKAZI MUHUMU



IKIWA zimebakia siku chache kuanza kwa zoezi la sense ya watu na makazi wananchi wa kata ya Kiwila wilayani Rungwe Mkoani Mbeya wameshauriwa kujiepusha na maneno mbalimbali yanayo ibuliwa na baadhi ya viongozi wa siasa ambao hawaoni umuhimu wa zoezo hilo.
   
Akizungumza na Rock Fm Diwani wa kata ya Kiwila Laulent Mwakalebule amesema kuwa pamoja na kwamba vyombo malimbali vya habari Radio Television na magazeti vinatangaza kuhusu mambo ya sensa baadhi ya wananchi wa kiwila hawaoni umuhimu wa zoezi lenyewe na kulichukulia vibaya zoezi hilo.

Hata hivo amesema kuwa watu wengi bado hawaja patiwa elimu kuhusiana na sensa kwani hiyo inatokana na takwimu kuchukuliwa na kucheleweshwa kutolewa kwa majibu.

Aidha mwakalebule ametoa tahadhali kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili wahesabiwe kwa ni takwimu na makazi ni muhimu kwa taifa.