MOMBA: WAZAZI WAOMBWA KUTOA USHIRIKIANO





WAZAZI wa wanafunzi wa shule ya msingi Usoche  kata  ya Kamsamba  wilaya  ya Momba  wamelalamikiwa na Mkuu wa shule hiyo kwa kuto toa ushirikiano na waalimu kwa watoto wao juu ya elimu.

Akizungumza  na  ELIMTAA  mkuu wa  shule  hiyo  Bw.  Leonard  Mwalunda  amesema  kuwa  wazazi  hawaonyeshi  ushirikiano  na walimu  wa shule  hiyo katika  kuiletea  maendeleo ya ufauru kwani wanafunzi  wamekuwa  wakienda  kuchunga  ngombe  na  kutohudhuria  vipindi darasani

Aidha  ameongeza  kuwa shule  yake  haina  walimu  wa  kutosha, madawati   pamoja  na  vitendea  kazi  ili  kuweza  kuiletea  maendeleo na ameiomba  serikali itupie macho  suala  hilo  ili  kuinua  kiwango   cha  taaluma  kwa  shule  hiyo.  

Habari Na  Yasinta Msuta