Polisi nchini Kenya
ilimtia nguvuni mwanamke mmoja mjini Nairobi
akiwa na bomu la kurushwa kwa mkono na bastola tatu.
Maafisa wa polisi wamesema kuwa mwanamke huyo, ambaye
jina lake halijatajwa, anashikiliwa kwa tuhuma za
kupanga mipango ya ugaidi na anatarajiwa kupelekwa mahakaman wiki hii.
Mkuu wa polisi wa mkoa wa Nairobi, Antony Kibuchi amesema mtuhumiwa
amekamatwa katika eneo la Rurii kwenye mashamba ya Zimarmani na anahojiwa na
kikosi maalum cha kupambana na ugaidi.
Polisi inajaribu kuangalia kama
kuna uwezekano wa kushirikiana na wenzake.
