GAZA: WAPALESTINA WAWILI WAUWAWA



Wapalestina wawili wameuwawa usiku wa kuamkia leo katikati mwa Ukanda wa Gaza kwenye shambulio la angani la Israel. 

Hayo ni kwa mujibu wa maafisa wa usalama wa Palestina. 

Maafisa hao wa chama chenye msimamo mkali cha Hamas kinachoutawala Ukanda wa Gaza wamezipata maiti za Wapalestina hao waliouwawa muda mfupi kabla saa sita usiku, karibu na mpaka na Israel, mashariki mwa Dieri al- Balah.