DODOMA: MNYIKA ATOLEWA BUNGENI BAADA YA KUKATAA KUFUTA KAULI





MBUNGE wa Jimbo la Ubungo John Mnyika ametolewa Bungeni baada ya kutoa kauli chafu na kukataa kuifuta kitendo ambacho ni kinyume cha kanunu ya Bunge ambayo inamtaka mbunge kufuta kauli pindi atoapo kauli chafu.

Mnyika ametolewa katika kikao hicho bunge la bajeti baada ya kutoa kashifa kwa Rais Kiwete kuwa ni dhaifu pamoja na chama chake kauli ambayo katibu wa Bunge, Job Ndugai akamtaka aifute na yeye kukataa kuifuta kauli hiyo.

Mnyika kuonyesha msimamo wa kile alicho kitamka hakutaka kufuta kauli na kisha kutoka bungeni pia Mh. Ndugai amesema kanunu za bunge ni muhimu kufuatwa kwa wabunge wote na ametolewa kwa kikao hicho na kuendelea kikao kinacho fuata.