DODOMA: WAKATI BUNGE LINAENDELEA WABUNGE WAANZA KUHOJI UTEKELEZAJI WA MABO MALI MBALIMBALI FUATANA NAMI


KUJENGWA ama kutojengwa kwa kivuko cha Mto Songwe kutategemea matokeo ya utafiti unaofanywa na serikali kwa sasa.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge ameliambia Bunge wakati akijibu swali la Mbunge wa Ileja, Aliko Kibona (CCM), wakati Mbunge huyo akitaka kujua lini serikali itakuwa tayari kujenga kivuko kwenye mto huo, ili kunusuru maisha ya raia na mali zao.

Akijibu swali hilo, Lwenge amesema kabla ya serikali kufikia uamuzi wa kujenga kivuko kwenye mto huo, wizara itatuma wataalamu katika mwaka wa fedha 2012/2013 ili kufanya utafiti, ikiwa ni pamoja na kujua kina cha maji ya kutosha ili kivuko kiweze kuelea wakati wote wa masika na kiangazi pamoja na upana wa mto.