Mpango huo unatoa wito kwa nchi 27 mwanachama wa umoja huo kukubali uamuzi wa mamlaka kwenye masuala ya fedha, bajeti na sera za uchumi kuhamishiwa kutoka miji yao mikuu hadi mjini Brussels katika kipindi cha miaka 10 ijayo.
Wakiwa chini ya shinikizo kutoka kwa washirika wenzao wa nchi za kundi la G20, nchi za Umoja wa Ulaya zinapambana ili kupata njia muafaka ya kuutatua mzozo wa kiuchumi katika kanda ya sarafu ya Euro.
