Uncategories
SYRIA:ANNAN APITISHA MKUTANO WA NGAZI ZA JUU
SYRIA:ANNAN APITISHA MKUTANO WA NGAZI ZA JUU
Mpatanishi wa Kimataifa kwenye mzozo wa Syria
Kofi Annan amedhamiria kuitisha mkutano wa ngazi ya juu kuhusu nchi hiyo mjini Geneva Jumamosi
ijayo kwa lengo la kutafuta msimamo wa pamoja kuhusu pendekezo alilowasilisha.
Msaidizi wake Annan, Jean Marc Guehenno
ametoa taarifa hiyo hii leo wakati akihutubia Baraza la Haki za Binaadamu la
Umoja wa Mataifa mjini Geneva.
Guehenno amesema kuwa Annan anafanya kazi na
mataifa pamoja na pande zote zinazohusika kwenye mzozo wa Syria ili
kuleta amani na utulivu lakini muda unakimbia.