Washauri wakuu wa waziri mkuu wa Uingereza wajiuzulu

Washauri wawili muhimu wa waziri mkuu wa Uingereza, Theresa May wamejiuzulu.
Pia kuna ripoti kwamba wanachama wakuu wa chama tawala cha Uingereza, cha Conservative, wametishia kuanza kutafuta kiongozi mpya, endapo washauri hao hawatotolewa kazini.
Mpambe wake, Nick Timothy, alisema anabeba dhamana kwa mchango wake katika kampeni ya chama, lakini alisema bado anaamini manifesto ilikuwa sawa, manifesto ambayo mwanachama mmoja maarufu alisema ni mbaya kabisa katika historia.
Msemaji wa chama amesema, mwenzake Bwana Timothy, Fiona Hill, piya amejiuzulu.
Bibi May anajaribu kuunda serikali ambayo haina wingi wa viti bungeni, kwa kutegemea chama kimoja cha Ireland Kaskazini.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r6U9vm
via IFTTT