Ndege ya Jeshi Yapotea na Watu 100 Ndani

BBC,Burma. Ndege ya jeshi la Burma, iliyokuwa imewabeba zaidi ya watu 100, imetoweka.
Taarifa zilizotolewa na viongozi wa kitaifa wa Burma, zimeeleza kuwa ndege hiyo ya kijeshi, ilikuwa imeruka kati ya Yangon (Rangoon) na mji ulioko Kusini mwa nchi hiyo wa Myeik. Shughuli za kutafuta ndege hiyo.
“Tulipoteza mawasiliano na ndege hiyo kuanzia saa 4:35 leo asubuhi (saa za Afrika Mashariki), ndege hiyo ilipofika maili 20 Magharibi mwa Mji wa Dawei,” jeshi la Burma limetoa taarifa hiyo
Inaelezwa kuwa ndege hiyo ilikuwa na abiria 105 na wafanyakazi 11.
Ndege za wanajeshi pamoja na helikopta zimetumwa katika eneo hilo katika shughuli za kuwatafuta manusura au mabaki ya ndege hiyo ambayo mpaka sasa inaaminika kuwa imeanguka.
Taarifa zinaongeza kuwa, ndege hiyo ilikuwa angani ikivuka bahari ya Andaman dakika chache baada ya kutoweka.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sXjcBz
via IFTTT