ASKARI POLISI AUAWA NA GARI KUCHOMWA MOTO KIBITI

Watu wasiojulikana wamemuua kwa kwa kimpiga risasi Askari Polisi wa Kikosi cha Usalama barabarani na kisha kuchoma moto gari alilokuwa analitumia.
Tukio hilo limetokea leo mchana katika Kijiji cha Bungu B wilayani Kibiti Mkoani Pwani ambapo vikosi vya usalama vilianza safari wakati huo kwenda eneo la tukio.
Jeshi la Polisi halijatoa taarifa yoyote hadi sasa kuhusu tukio hilo.
Tukio hili limetokea ikiwa ni saa chache tangu Rais Magufuli aliposema kwenye mkutano wa hadhara Mjini Kibaha kuwa wahalifu hao katika Wilaya za Kibiti na Rufiji wameanza kushungulikiwa na moto wameupata.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2tR5nVD
via IFTTT