WASCOTLANDI WALIVYO JITOA KUSAIDIA ELIMU NJOMBE

“ALICHAGULIWA  na chifu, Joseph Mbeyela  kuwa aje kugombea ubunge waka 1975 akiwa na wasomi wengine lakini yeye ndio alipita kutokana na alivyo kuwa mtu mvumilivu na mpendamaendeleo,"

Hiyo ni kauli ya mkurunzi wa Taasisi ya aliyekuwa mbunge wa jumbo la Njombe kwa miaka 35 kuanzia mwaka 1975  marehemu Mh. Dr. Jackson Mwakwetta ambayo ni Jackson Makwette Foundation.

Mkurugenzi Jocktan Muhomisoli anasema kuwa mbunge wa jimbo la Njombe miaka 35 kuanzia mwaka 1975 alikuwa ni mbunge aliyeitwa na chifu wa wabenda ili aje kuwaongoza wakazi wa jimbo hilo la Njombe ambalo lilikuwa na miji mikubwa ya Ludewa, Makete na Njombe yenyewe.

“Chifu  Mbeyela alimwita Dr. Makwetta kwajili ya kuja kugombea jimbo la Njombe na kuwasaidia wananchi wa jimbo la anajombe kwa wakati huo, alisema kuwa hakutaka jimbo liongozwe na watu wasio na elimu alimwita kwa kuwa alikuw ani mutu mwenye elimu ya juu," alisema Muhomisoli .

Dr. Makwettta aliitwa na Chifu Mbeyela akiwa katika chuo cha Mzumbe akifundisha huko na chifu alisema kuwa niitieni kwa kuwa aliujua usezo wake.

"Kabla Dr. Makwetta hajawa mbunge haja wa mbunge aliitwa kutoka mzumbe na chifu kuja kugombea ubunge, chifu alisema kuwa niitieni yule kwa kuwa uwezo wake aje hapa agombee kwa kuwa nataka jimbo hili liongozwe na mtu mwenye elimu na uwezo wa juu," alisema Muhomisoli .

Alisema kuwa Dr. Makwetta likuwa ni miongoni mwa watu, wabunge walio kuwa wakipenda kufanya maendeleo na kusababisha jimbo lake kuwanza kupanda miti kwaajili ya biashara baada ya kuwa mbunge kwa kuwa miaka hiyo ya nyuma watu walikuwa wakiiona mitu katika maeneo ya misheni tu.

“Siku moja Dr. Makweta alikuja katika shule Lwanzali ambayo nilikuwa nafundisha wakati tu ndo ameanza ubunge wake aliwaambia waalimu pale shuleni kuwa Mwalimu ametupitishia reli ya Uhuru hapo jirani lakini sisi haitusaidii kwa maendeleo shule andaeni vitaru vya miti ili tuanze kupanda miti," alisema na kuongeza kuwa

"Alikuja na mbegu za miti shule iliandaa miche ya miti na watu wakaanza kupanda miti kwa kuchukua mbegu shuleni baada ya shule kupanda miti ya kutosha na mbegu kubaki ambapo mbegu ziliandaliwa na mabwana shamba," aliongeza Muhomisoli .

Baada ya kuanzishwa kwa upandaji wa miti katika jimbo la Njombe basi miaka ya 1986 katika maeneo ya Makambako kulianza na wafanyabiashara kung'ang'aniana mbao ambazo mzilikwenda sehemu mbalimbali za nchi kwa njia ya Reli ambapo baada ya kuonekana kuna uzalishaji wa mbao kwa wingi basi kukajengwa mpambo mkubwa kwaajiuli ya kupakulia mbao kutoka kwenye magali na kupakia katika Treni.

“Mwaka 1986 mbao zilianza kuvunwa na wakazi wa Njombe  kuanza kufurahia matumizi ya reli na wafanyabiashara akubwa kuchukua mbao kutoka Njombe na kwenda kuuza maeneo mengine ya nchi wazo ambalo lilitolewa na Mbunge,"

Muhamisoli anasema kuwa Dr. Makweta alikuwa waziri katika wizara nane hapa mchini ikiwamo wizara ya Elimu, na alikuwa katika utawala wa Hayati Mwalimu Juliaus Nyerere, Rais Mstaafu Ally Hassan Mwuni na Rais Mstaafu Benjamini Mkapa bila kukumbwa na kashifa yoyote kwa Kipindi hicho.

Miaka ya nyuma kidogo Dr. Makwetta akiwa Mbunge mtoto wake alikwenda kusoma nje ya nchi katika nchi ya Scotland ambako alikutana na wanachua ambao walikuwa na mfumo wa kwenda kusaidia nchi furani kutokana na michango yao.

Wanafunzi hao wenzake wa mwanae Dr. Makwetta ambaye alikuja kumuliza baba yakje kuwa je kuna watu wanatoa misaada mbalimbali kwa nchi tofauti duniani wanaweza kuja, akiwa mbunge aliwaruhusu watu hao kuja kusaidia Njombe kwa maendeleo.

Watu hao walikuwa wakijichangisha fedha na kukushanya kwa kufanya michezo mbalimbali na kucheza disko pesa zikipatikana wanazikusanaya na kunda kutoa misaada kabla ya kuja Tanzania walikuwa wanasaidia nchi za Mashariki ya mbali.

“Wanachuo wa chuo kimoja huko Scotland walikuwa wanafanya michezo yao mbalimbali na kukusanya fedha na kwenda kusaidia nchi mbalimbali hapa duniani mwanae Dr. Makwetta aitwae Atwitye aliamua kuwa kuwashawishi wanafunzi wenzake ili kuja kusaidia hapa nchini ambapo baada ya kuja hapa nchini walianza kufanya misaada mbalimbali chini ya Mbunge " alisema Muhomisoli .

Wanafunzi hao ambao walikuwa wakifanya hivyo kala unapo baki mwaka mmoja kumaliza chua walianza kupokelewa na Mbunge kwa miaka hiyo na kufanya ujenzi wa miradi mbalimbali ya kijamii ambapo walisaidia ,masuala ya kielimu.

Walifanya ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondali Manyunyu kunakajengo walijenga hao vijana, shule ya sekondali Tipingi pia walijenga maabara, Pia katika shule waliyo ipa jina lake mwenyewe Jackson Makweta nako walitoa misaada na walikuwa wakitoa misaada kwa nyakato tofauti.

Sasa mwaka wa kwaza kuja baada ya kufaliki mwaka 2012 marehemu Dr. Makweta waliamua kutembelea kijijini kwakwe ambako walitaka kujua kile alicho kifanya kijijini kwake enzi za uhai wake.

“Waliamua kutembelea kijijini kwake ambako kwa hali walio ikuta waliamua kujenga ukumbi wa kulia chakula katika shule ya Muhaji," alisema.

Wascotland hawa walijifunza kuwa shule za hapa kwetu hazina vimba vya kompyuta basi wakajenga chumba cha kompyuta katika shule hiyo na mwezi Juni mwaka huu wanaleta Kopyuta kwaajili ya wanafunzi kujifunza.

“Ahadi ya wascotlandi ni kuisadidia Njombe miaka mingi ijayo katika maendeleo kama walivyo patana na marehemu Dr. Makweta enzi za uhai wake, pia wameamua kujenga ukumbi mkubwa pale nyumbani kwa marehemu," aliongeza Muhomisoli.
 
Kwa mara ya kwanza baada ya kifo cha Dr. Makwetta walipokelewa na Mkewe na kuwatembeza katika miradi yote waliyo kuwa wakiifadhiri lakini ikagundulika itakuaje kufanya mama peke yake wakati watu hawa wamedhamili kutoa misaada miaka mingi basi kukaanzishwa Jackson Makwetta Foundation.

Anasema kuwa lengo la kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni kuhakikisha kuwa wanapatikana wakina Makweta wengine watakao isaidia Njombe kwa kushilikiana na Wascotland hao basi taasisi hiyo imeanza kwa kuchukua wanafunzi wanne ambao hawana msaada wowote kuwasomesha shule kama watakuwa na uwezo basi mpaka kufika vyuo vikuu.

Alisema taasisi ina chukua wanafunzi hao kwa kushirikiana na serikali ya kijiji kwaajili ya uhakikika wa mtoto  anahitaji msaada kweli na watoto hao wanne kutoka katika shule ya msingi Mhaji.

Watoto hao wanapewa vifaa vya msingi na kuwapatia upana wa akili kwa kuwatembeza maeneo mbalimbali huku kuwasaidia ni wale wenye uwezo tu lakini pia watoto wengine wanne wanaendelewa ni kutoka shule ya sekondari Jackson Makwetta.

Muhomisoli anasema siasa ya miaka ya hivi karibuni imejawa na watu wenyepesa watu wanaingia kwa kuhonga pesa tofauti na miaka ya nyumba ndio maana hakuna uadilifu na maendeleo yanakuwa ni hafifu kwa wananchi.

Sasa utakuta watu wanachaguliwa kwa mpaka wawanunulie ulanzi ndipo wanamchagua mtu huyu akiingia madarakani lazima afanye wizi ili kulipia zile Rushwa alizo zitoa.

Ili kuyaenzi yale aliyoyafanya mbunge aliyeteuliwa na chifu navkurithisha kwa kizazi hiki Mwenyekiti wa bodi Atwitye Makwetta anawaomba wadau kuwasiliana na taasisi kwa barua pepe jm.found@gmail.com.

Makala hii imeandaliwa na Furaha Eliabu, mwandishi wa habari anapatikana,kwa email: furahanews@gmail.com, simu 0753321191,