Wafanyakazi wajitokeze kwenye kupiga kura

SERIKALI Mkoani Njombe imewataka wakazi wa mkoa huo kuhakikisha wanajitoikeza kwa wingi kupigia kura Katiba Pendekezwa kama walivyo jiandikisha katika Daftari la kudumu la mpiga kura itakavyotakiwa kuipigia kura.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Njombe, Sarah Dumba wakati wa maadhimisho ya siku ya mfanyakazi ambapo wafanyakazi Mkoani Njombe wameungana na wafanyakazi kote duniani kuadhimisha siku hiyo.

Dumba amesema kuwa wananchi na wafanyakazi wanaotakiwa kujitokeza kwa wingi kuipigia Katiba Pendekezwa kura ya ndio itakapo tangazwa siku ya kuipigia kura.

Kwa upande wao wafanyakazi wamesema kuwa wanaomba mkoa huo ili kuboresha Maendeleo ya mkoa ni vyema miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara, mabweni na hospitali.

Akisoma taarifa ya wafanyakazi kwa mkuu wa wilaya Katibu wa chama cha walimu wilaya ya Njombe Salama Lupenza alisema kuwa mkoa ili kupata Maendeleo unahitajika kuwa na wasomi na kuwa mkoa huo unawajibu wa kuhakikisha unajenga mabweni kwa shule zake ili kuendeleza kushika nafasi za juu kielimu kama ulivyofanya mwaka huu.


Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika halmashauri ya Njombe kimkoa na kuhudhuliwa na mamia ya wafanyakazi kutoka wilaya mbalimbali wa mkoa huo wafanyakazi wameitaka serikali kuongeza kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi ili kuweza kuyamudu maisha.