Vituo vya kazi kuto kuwa na malazi vyakimbiza watumishi, Njombe

KUTO kuwapo kwa makazi imara katika kata mbalimbali hapa nchini kumedaiwa kukwamisha watumishi kufika kufanyakazi katika kata za pembezoni wakikimbilia mjini kwenye makazi imara ya kuisha.

Hayo yamebainishwa na Diwani wa kata ya Makowo halmashauri ya Mji wa Njombe Ojen Mdete wakati Akizungumza katika baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo na kuwa kata yake watumishi katika kituo cha afya hufika na kuodoka kutokana na makazi ya hadhi ya kukaa watumishi hao kuto kuwapo.

 Amesema kuwa suala hilo limesababisha kuto kuwapo kwa huduma katika kata yake kutokana na watumishi katika kituo cha afya kuto kuwapo.

Mdete amesema kuwa watumishi wamekuwa wakifika na kukaa siku chache na hatimaye kuondoka na kusikia wamepangiwa kata mahara pengine na kuwatupia rawama maafisa utumishi kwa kuwahamisha watumishi katika kata yake.


Ameongeza kuwa watumishi wanapo omba uhamisho kuhakikishwe kuwa wanaona kuwa amapo toka kuna mtu anaye mbadala pale kabla ya kuondolewa mtumishi huyo ili kutoacha vituo vya kazi bila watumishi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la Madiwani halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga amesema kuwa wananchi wanawajibu wa kushirikiana na Madiwani wao kuhakikisha miundombinu ya kuishi watumishi inaboresha ili watumishi wanapoingia katika vituo vyao vya kazi hawatamani kuhama.

Amesema kuwa watumishi isionekane wanakataa mazingira waliyo pangiwa kazi bali na mazingira Yao ya kufanyia kazi yatazamwe yakoje kwani kuna mazingira ambayo watumishi wakipelekwa hayafai kuishi hata afisa utumishi akipelekwa pale hawezi kuishi mazingira ni duni kupita kawaida.