Sensa ya viwanda yaanza Njombe



SEKTA ya viwanda hapa nchini ni sekta ambayo ina muhimu katika Maendeleo kutokana na ajira zinazo tokana na sekta hiyo na mapato yanayo tokana mapato ya viwanda.
Sasa setikali inatakiwa kujua kuna viwanda vingapi na mapato yake, ukuaji wake na kujua uendeshaji wake.
  

Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Njombe Meneja msaidizi wa ofisi ya takwimu ya taifa mkoa wa Njombe na Iringa  Respicius Gasper amesema kuwa serikali inatarajia kufanya utafiti katika viwanda hapa nchini.



Ameongeza kuwa takwimu hizo zinalenga kuboresha sera ya viwanda hapa nchini na kujua viwanda vingapi vipo hapa nchini na zoezi hilo limefanikiwa kwa asilimia kadhaa na kuwa kunachangamoto wanakabiliana nazo kama anavyo eleza.


Amesema kuwa takwimu zinazo kusanywa hazihusishwi na mamlaka yoyote ile na kuwa zitakuwa ni kwaajili ya ofisi hiyo huku akiwaomba wamiliki na wahusika wa zoezi hilo kuhakikisha kuwa wanatoa ushirikiano kwa watakwimu.