Maduka kufungwa siku tatu mfululizo, ni Juni 8 hadi 11

JUMUIYA ya wafanyabiashara Mkoani Njombe inatarajia kuambatana na wafanyabiashara wote Mkoani humo kuelekea mjini Dodoma kwenda kusikiliza kesi ya kiongozi wa jumuiya hiyo kitaifa Jonson Minja.

Inadaiwa kuwa wafanyabiashara Mkoani humo watafunga maduka na kwenda mjini Dodoma kusikiliza hiyo ambayo itaendeshwa kwa siku tatu mfurulizo ambapo inatarajia kuanza Juni 8 hadi 11.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa jumuiya hiyo mkoa wa Njombe, Sifaeli Msigala hivi karibuni baada ya baada ya kumaliza kesi ambayo ilikuwa inamkabili Mfanyabiashara mwenzao Mexsons Sanga.

Alisema kuwa ataungana na wafanyabiashara wote nchini kuelekea Dodoma huku maduka yakiwa yamefungwa kwa siku tatu mfurulizo.


Wafanyabiashara wameafikiana kufunga maduka kwa siku hizo tatu huku wakikemea wasalili ambao wanafungua maduka wakati wanakwenda mahakamani.

“Wale watakao kuwa wakikweba kodi na huku wapo katika jumuiya hatuta kubaliana nao kwa kuwa jumu iya hii sio kwaajili ya kukumbia kodi kazi yake ni kusimamia kodi zote hapa nchini,” alisema

Alisema kuwa kuwapo kwa jumuiya hiyo ni kuhakikisha kuwa kodi inaliopwa na wafanyabiashara wanafuata kanuni za biashara ili kuto ikwaza serikali na kuhakikisha nchi inaendelea na kuwa watapambana na wenzao watakao kwepa kodi.

Aidha Mexsons alisema kuwa tangu awali mkoa wa Njombe ulijulikana kama shamba la bibi kutokana na upole wa wakazi wa mkoa huo kitu ambacho hakikuwa maana ya wakazi hao.

“Wakazi wa Njombe zamani TRA walijiwekea kuwa ni shamba la Bibi ambapo walikuwa wakija na kujichukulia pesa na kwenda kufanya maedeleo huko ndomana utaona wafanyabiashara wengi walikuwa wanainuka na kushika, lakini sasa tuamke tuache kutoa rushwa,” alisema Mexson

Aliongeza kuwa wakazi hao pia walikuwa wakiogopa mamlaka ya mapato tanza nia TRA na wengine kuogoma kufanya Maendeleo na baada ya kesi yake majengo ya ghorofa kuanza kujengwa.

“Mkoa huu watu walikuwa na fedha zao nyingi tu walikuwa wanaogopa kusimamisha ghorofa unaona sasa gorofa zinajengwa baada tu ya mimi kuamka na wao TRA sasa wanaogopa kuja watu wanajenga sasa,” alisema Mexsons