Abiria wapatashinda Njombe

ABIRIA wa kwenda maeneo mbalimbali kutoka Mkoani Njombe wameshindwa kusafiri kutokana na mgomo wa madereva unaoendelea Mkoani hapo huku wakiitupia lawama serikali kuto wasikiliza madereva hao.

Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti Mkoani hapo wamesema kuwa kuto kuwapo kwa usafiri kutokan ana mgomo huo ni aibu kwa serikali kwa kuwa mgomo huo ni tabu kwa wananchi.

Mmoja wa wasafiri kutoka Mkoani Mbeya na kuelekea Mkoani Songea, John Mapunda alisema kuwa hali hiyo ni kero kubwa kwa wananchi na kuwa serikali iwasikilize madereva ili gari zianze kufanya kazio yake za usafirishaji.

Alisema kuwa mgomo huu unawaadhili sana watu wenye kipato cha chini kwa kuwa watu wasiposafiri wanaweza kulala nje kwa kuwa kunawengine walikuwa wanasafari na wamefikia katikati ya safari na pesa kushindwa kuelekea popote pale na poesa walizo nazo kidogo.

Aidha Abel Ngolochemba alisema kuwa yeye anatokea Makambako kwenda Njombe mjini na kutumia usafiri wa Noah na kuwa wametozwa pesa kubwa kutoka nauli ya kawaida ya shilingi 2500 na kulipa 6000, na kuwa serikali itaadhirika kutokana na wafanyakazi kufika katika ofisi zao kwa kuchelewa.

Alitoa ushauri kwa serikali kuwasikiliza madereva na kuwa isipo wasikiliza kuna watu watakufa kutokana na mgomo huu na wengine kukosa huduma muhimu ambazo ilitakiwa kuzipata kwa kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Kwa upande wao madereva walisema kwua serikali inatakiwa kuwaita madereva wamesema kuwa wanaotakiwa kukaa na madereva kwa kuwa kuto kuwapo kwa  madereva ambao ndio wanagona na kukaa baadhi yao.

Mmoja wa dreva ambaye hakutaka kujajwa jina lake alisema kuwa mgomo huo upo sahihi lakini serikali kitendo cha kuwalazimisha kusoma mara kwa mara ni kitu ambacho hakizezekani kwa kuwa elimu haitapunguza ajali na kuwa ajali hizo njingi zao zinasababishwa na madereva wa maroli.

Alisema kuwa serikali ilitakiwa kujadili baina ya madereva na wadau wengine na kuwa isikae na maafisa wa polisi pekee ili madereva waseme nini kinawasumbua na nini kina sababisha ajali.

Alisema kuwa madereva wanaolalamikiwa ni bora wangewaita na madereva wa maroli kwa pamoja na kuwa ajali zingine zinasababishwa na ubovu wa miundombinu, na kuwapo kwa baadhi ya Trafiki wa tochi wakijifiucha na kujitokeza barabarani kwa ghafla.


Alisema kuwa serikali kuhusu kusababisha ajali ni bora ikaangalia usalama kwaza kuliko mda wa kufika safari zao inatakiwa kuangalia kuwa wamefika salama na kuwa kuangalia wanafika salama bila kujali mda.

Kwa habari zaidi Piga (For More Call us) +255656049045