Ghasia za ubaguzi zapingwa Afrika Kusini (Habari Kamili)


Waandamana kupinga ghasia za kibaguzi dhidi ya wahamiaji Afrika kusini
Maelfu ya raia katika mji wa mashariki wa Durban nchini Afrika Kusini wanaandamana kupinga ghasia za hivi majuzi dhidi ya wageni.
Takriban watu watano wameuawa tangu wiki iliopita katika ghasia dhidi ya wahamiaji ambao wameshtumiwa kwa kuchukua kazi za raia wa taifa hilo.
Hofu ya kusambaa kwa ghasia inaendelea kutanda.
Raia aliyejeruhiwa kutokana na ghasia dhidi ya wageni Afrika kusini
Mjini Johannesburg ,wamiliki wa maduka kutoka mataifa ya Ethiopia,Somalia na mataifa mengine ya Afrika wamefunga biashara zao wakihofia kuporwa.
Rais Jacob Zuma wa Afrika kusini ameshtumu ghasia hizo na anatarajiwa kulihutubia bunge baadaye.
Mnamo mwaka 2008 watu 62 waliuawa kufuatia ghasia za kibaguzi zilizokumba taifa hilo.