Wakulima kupata kinga ya ardhi kikatiba


Kwa Kiingereza Bofya hapa

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais uratibu na Mahusiano Sephen Wassira, amesema kuwa katika katiba mpya kunatarajiwa kuwekwa kipengele kitakacho iweka ardhi kisheria na kutambulika kama rasilimali ya taifa.
 
Akizungumza katika maonyesho ya Nanenane baada ya kutembelea mabanda mbalimbali katika viwanya Vya maonyesho hayo vya Nzuguni mjini hapa, Wassira ambaye ni mwenyekiti wa moja ya kamati za bunge la katiba, alisema kuwa katika katiba hii kumejadiliwa kibengele kitakacho ilenga ardhi na kuwema mamlaka zitakazo simamia moja kwa moja.

 Alisema kuwa itakuwa hivyo kwa sababu ardhi ndio msingi wa maisha ya mtanzania kwani maliasili zote zipo ndani ya ardhi.

“Shabaha ni kuweka katika sura ili katiba ielekeze mamlaka zitakazo simamia juu ya namna rasilimali za taifa zitakavyo simamiwa kama vile gesi, Ardhi na maliasili zingine zilizopo chini ya ardhi, Alisema Wassira.
  
Alisema kuwa bunge hili kabra halija malizika linatarajia kushugulikia mambo hayo kabla halijamalizika kuhakikisha kuna kuwepo kwa sura hiyo katika katiba mpya.

Alisema kuwa jambo hilo litakuwa ni hakikisho kwa wakulima kwani ardhi itapata msimamizi mwenye nguvu na kuipa ardhi umuhimu wa hali ya juu kuliko ilivyo hivi sasa.

Aidha Wassira alisema kuwa yeye kama Mwenyekiti wa kamati namba sita kamati yake mpaka sasa imejadili sura tatu na kuwa ilitakiwa kufika juma tatu wawe wajadili sura nne.

Hivyo katika kamati yake katika kamati yake ambayo juma tatu inaanza sura ya nne, alizitaja sura ambazo tayari zimejadiliwa katika kamati yake kuwa ni pamoja na sura inayo husu sera za jumla za taifa ambazo zitakuwa ni msingi wa kutengeneza sera na sheria za nchi.

Alisema mbali sura hiyo pia wamejadili sura ya Tatu ambayo inazungunzia maadili na miiko ya viongozi itakayo wazibiti wanao penda kutafuna mali za wananchi.

“Kumekuwa na baadhi ya watu wakipatiwa nafasi ya uongozi wamekuwa wakiwaza kutafuna mali za wananchi na badala ya kuwaza wataiingizia nchi nini katika uongozi wao, katika majandiliano yetu tumeweka vifungu katika katiba vitakavyo wabana watu wanao tumia vibaya rasilimali za taifa,” Alisema Wassira  

Kuhusiana na wajumbe kuingia walio toka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) Wassira amesema kuwa katika kamati yake hawajapokea mgeni yeyote kutoka nje ya walio ingea ile siku ya kwanza.

Alisema kuwa yeye hana shida na wajumbe hao na waendelee kurejea katika bunge hiro na nibusara kurudi katika bunge hilo ni jambo la busara.

“Naona ni busara kuendelea kurudi katika Bunge ra katiba kwani naona wanavyo fanya wale wanao wakemea wale wanaonaoendele kuingia katiba bunge la Katiba,” Aliongeza Wassira.