Ndege iliyo anguka Iran yaua watu 40



Ndege ilioanguka nchini Iran

Ndege moja iliokuwa na abiria 40 imeanguka mjini Tehran nchini Iran.
Runinga ya taifa la Iran imesema kuwa abiria wote wamefariki .
Ndege hiyo ya kampuni ya Taban Air imeripotiwa kuanguka katika makaazi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Mehrabad Maghribi mwa mji wa Tehran.
Ndege hiyo inayojulikana kama Iran 141 ilitengezwa nchini Iran kupitia teknologia ya Ukraine.
Uchunguzi umeanzishwa kuhusu ni nini kilichosababisha ajali hiyo.
Iran imekabiliwa na ajali kama hizo katika siku za hivi karibuni kutokana na ndege zake zilizozeeka mbali na marekebisho mabaya inazozifanyia.