NHIF KUKUTANA NA WADAU WAKE MKOANI MBEYA

WAKURUGENZI wa halmashauri na watendaji serikalini wametakiwa kuwahimiza wananchi wa kujiunga na mfuko wa jamii wa afya (NHIF) ili kujikinga na masuala ya magonjwa na kufikia malengo ya kusajili kaya nyingi.

Hayo yamebainishw ana mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandolo, alisema kuwa wakurugenzi waweke mikutano ya kuhamasisha wananchi kujiunga na NHIF na kuulizana kwanini wanachama hawaongezeki.

Amesema kuwa wakurugenzi na watendaji katika halmashauri mkoani mbeya wajitahidi kufika katika kila kona ya halmashauri ili kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo.

Alisema kuwa kuwa halmashauli nzitenge fedha kwaajili ya kutoa elimu kwa wananchi  juu ya umuhimu wa kijiunga na taasisi hiyo ya kiafya.

Alisema halmashauri pia zichukue hatua ya kuhakikisha vituo vinavyo toa huduma kutoa huduma bora kwa wateja wanaohuduma.

 Alisema kuwa wananchi wakijiunga na mifuko hii itawasaidia wananchi watakao ugua kupata hudiuma hiyo hata kama hana pesa.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi mwezeshaji wa NHIF Grece Lobulu alisema kumekuwa na ongezeko la taratibu kwa wananchi wanao jiunga na mfuko huo.

Alisema kuwa asilimia kumi na moja mkoani Mbeya wameongezeka na kwa mwaka ujao wanahitaji kuwafikia wananchi wengi ili kufika mwaka 2015 kuwafikia wananchi wengi hadi asilimia 35.

Amesema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali za baadhi ya wananchi kutumia kadi moja kwa wananchi  zaidi ya mmoja na wanajitahidi kukabiliana na changamoto hiyo.