MAJESHI YA SYRIA YASONGA MBELE

Jeshi  la  Syria  limepiga  hatua  kuelekea  katika  maeneo yanayoshikiliwa  na  makundi  ya  Kiislamu  katika  kijiji  cha kaskazini  cha  Tal Hassel, wakati  waasi  wa makundi  ya  Jihad karibu  na  Aleppo  wakitoa  wito  wa  kupata  wapiganaji  zaidi  ili kuzuwia  hatua  hiyo. 
Mapigano  yameendelea  katika  kijiji  cha Tal Hassel, kilichoko kilometa 12 kutoka Aleppo, mji  wa  kale  wa kibiashara  nchini  humo. 
Kwa  mujibu wa shirika rasmi  la habari la SANA, katika maeneo mengine nchini humo mapigano yameendelea na watu tisa  wameuwawa  kwa  makombora  katika mji wa kati wa Homs. 
Afisa wa jeshi amethibitisha kuwa jeshi hilo  linaelekea katika kijiji cha  Tal Hassel, na  kuongeza  kuwa  jeshi  linatanua operesheni kuyachukua tena majimbo  yanayodhibitiwa na waasi.