MLIMA MBEYA |
Mtu huyo aliyejeruhiwa, Yohana Mdewa (54) inadaiwa
alikumbwa na mkasa huo kutokana na kudaiwa kuwa kihelele kwa kuwaongoza maofisa
hao wa halmashari kwenda kuwaondoa wananchi hao kwa kufyeka mazao yao
mashambani.
Tukio hilo lilitokea juzi katika kijiji cha
Isengo, kata ya Iziwa, wilayani Mbeya vijijini, ambapo kundi la wananchi
wapatao 400 kujikusanya na kuwavamia maofisa hao waliokuwa wakiendesha zoezi la
kuwaondoa wananchi hao.
Inadaiwa kuwa zoezi hilo halali la serikali
la kuwaondoa wananchi hao lilianza Januari 24 mwaka huu baada ya maofisa zaidi
ya 20 kutoka katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya na halmashauri ya Jiji, wakiwa
na mgambo kuvamia kijiji hicho na kuanza kufyeka mazao.
Habari zaidi zinadai kuwa baada zoezi hilo
kufanyika, juzi maofisa hao walirudi tena kwa lengo la kuendelea na oparesheni
hiyo, lakini ghafla walijikuta wakivamiwa na kundi la wananchi na kuanza
kushambuliwa kabla ya kukimbia na kwenda kujifungia kwenye ofisi za kijiji.
Taarifa hizo zinadai kuwa salama ya viongozi
hao ilitokana na jeshi la polisi kupata taarifa mapema na kupeleka askari
polisi 20 wakiwa na silaha za moto hali iliyoimarisha ulinzi katika ofisi hizo
kabla ya kuwaondoa.
Hata hivyo inadaiwa kuwa wakati polisi
wakiwaokoa maofisa hao, baadhi ya wananchi walirudi na kwenda kumalizia hasira
zao kwa kuyaharibu magari yaliyokuwa yamewabeba na kuwadfikisha kijijini hapo
maofisa hao wa halmashauri hizo na mgambo.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Diwani
Athumani, alipohojiwa juu ya tukio hilo alikiri kutokea, huku akisita kueleza
kama kuna watu wamekamatwa kwa kuwa jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wa
kuwabaini vinara wa mpango huo.
Alisema katika tukio hilo, ofisa mmoja kuoka
asasi ya kiraia ya utunzaji wa mazingira alijeruhiwa na mali ambazo ni magari
ya serikali yaliharibiwa vibaya na wananchi katika vurugu hizo zilizodumu kwa
zaidi ya saa mbili kabla ya jeshi hilo kufanikiwa kudhibiti.
Aliyataja magari yaliyoharibiwa kwenye vurugu
hizo kuwa ni STJ 1830 mali ya wakala wa hifadhi ya misitu nyanda za juu kusini,
ambalo lilipasuliwa kioo cha mbele,pamoja na kwa STJ
1821 na STJ 1832.
Aidha, Diwani alisema katika kile
kinachoonekana kuwa wananchi hao walikuwa wamejipanga kwa ajili ya vitendo
hivyo vya uhalifu, walitumia mbinu kali ya kubomoa madaraja mawili katika barabara
inayoingia kijijini hapo, baada ya msafara wa viongozi wa oparesheni kupita kwa
lengo la kuwadhibiti pindi mapambano yatakapoanza.
Kutokana na hali hiyo, kamati ya ulinzi ya
wilaya hiyo ililazimika kukutana ghafla kwa lengo la kuzungumzia mustakhabali
wa tukio hilo, ambapo walifikia maamuzi ya kuwa zoezi hilo lazima liendelee kwa
ajili ya kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji.
Hifadhi za msitu wa safu za mlima Mbeya (Mbeya
range forest reserve),zilitangazwa lasimi kuwa hifadhi ya akiba katika gazeti
la selikali mwaka 1957, ambapo kwa muda wote huo limekuwa likitumika kama
chanzo kikubwa cha vyanzo vya maji katika halmashauri hizo mbili za Mbeya Jiji
na Vijijini.
Kwa mujibu wa taarifa za pia wakala wa hifadhi ya misitu nyanda za juu
kusini, hifadhi hiyo ya msitu ulikuwa na vyanzo vya maji vya kuaminika 40,
lakini kutokana na uvamizi uliofanywa kwa muda mrefu na wananchi, kumebaki na
vyanzo 18 tu.
Mwisho.