MAPATO NA MATUMIZI NI MSINGI KWA TAASISI YOYOTE


KEMEKUWA na serikali nyingi za vijiji ambazo hazisomi mapato na matumizi ya fedha na kutokuwa na miradi ya ambayo itaingiza mapato katika vijiji vyao.

Serikali nyingi za vijiji hapa nchini zinashidwa kufanya mambo ya kimaendeleo kutokana na kutokuwa na mradi inayo igiza pesa katika mfuko wa kijiji hatimaye kushindwa kusoma taarifa za mapato na matumizi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake menyekiti wa kijiji cha Ruanyo kata ya Igurusi wilayani Mbarali mkoani Mbeya, Righton Mwakitwange, alisema kuwa katika kijiji kukiwa na mradi unao kisaidia kupata pesa kinaweza kuendelea kirahisi hivyo kuwapo ulazima wa kusoma mapato na matumizi.

Alisema kuwa Jumatano ya wiki hii katika kijiji chake anatarajia kusoma mapato na matumizi katika mkutano wa hadhara kijijini hapo.

Mwakitwange alisema katika mkutano hua anatarajia kujadiliana na wananchi kuunda miradi mbalimbali ya kuipatia halmashauri ya kijiji hicho ambapo mpaka sasa uongozi wa kijiji una mpango wa kujenga eneo la kuegesha magari makubwa.

Hivyo katika mkutano huo watalileta suala hilo kwa wananchi ili wajue kuwa kutakuwa na ujezi wa kitegauchumi hicho ambacho kitaingiza fedha katika kijiji na halmashauri ya wilaya ya Mbarali.

Alisema ujezi wa eneo hilo la kuegesha magali lita saidia watu wengine kuwekeza katika huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo nyumba za kulala wageni na maduka mbalimbali na vijana kupata ajira.

Katika kijiji hicho ambacho hakina vitegauchuni vya kutosha amesema kutokana na upungufu huo wamekuwa wakikwama katika ujenzi wa shule ya kijiji ambayo mpaka sasa wamejenga madarasa ambayo kwa sasa inahitajika kuezekwa nipo walipo kwamia.

Alisema kama kijiji kingekuwa na miradi ya kutosha wangeweza kukamilisha ujenzi wa shule hiyo mapema na amewataka wananchi  ambao ni wakazi wa kijiji hicho walioko nje ya Mbeya wajitokeze katika uchangiaji wa kijiji chao na kufanya maendeleo kusonga mbele.
mwisho