Kundi la wanaharakati nchini Syria limesema kuwa yamefanyika
mauaji mapya jana katika jimbo la kati la Hama.
Uongozi wa baraza la mapinduzi la Hama umeliambia shirika la habari la Reuters kuwa kijiji kinachoishi Waislamu wa madhehebu ya Sunni cha Taramseh kilishambuliwa kwa helikopta za kijeshi pamoja na vifaru na kwamba wanamgambo wanaoiunga mkono serikali wa kabila la Alawii baadaye walivamia kijiji hicho na kufanya mauaji ya kikatili.
Idadi ya watu waliouwawa inakuwa vigumu kuithibitisha nchini Syria, nchi ambayo serikali inazuwia waandishi habari kwenda katika maeneo mbalimbali. Wakati huo huo, mjini New York, baraza la usalama la umoja wa mataifa linaendelea kuvutana kuhusiana na azimio kuhusu hali ya baadaye ya ujumbe wa umoja wa mataifa nchini Syria ambao umeingia katika mzozano. Uingereza, Marekani, Ufaransa, Ujerumani na Ureno zinataka azimio ambalo litaweka muda wa siku kumi kwa Assad kusitisha mashambulizi yake ama akabiliwe na vikwazo chini ya ibara ya 7 ya mkataba wa umoja wa mataifa.
Urusi inakataa madai ya mataifa ya magharibi ya vikwazo.
Uongozi wa baraza la mapinduzi la Hama umeliambia shirika la habari la Reuters kuwa kijiji kinachoishi Waislamu wa madhehebu ya Sunni cha Taramseh kilishambuliwa kwa helikopta za kijeshi pamoja na vifaru na kwamba wanamgambo wanaoiunga mkono serikali wa kabila la Alawii baadaye walivamia kijiji hicho na kufanya mauaji ya kikatili.
Idadi ya watu waliouwawa inakuwa vigumu kuithibitisha nchini Syria, nchi ambayo serikali inazuwia waandishi habari kwenda katika maeneo mbalimbali. Wakati huo huo, mjini New York, baraza la usalama la umoja wa mataifa linaendelea kuvutana kuhusiana na azimio kuhusu hali ya baadaye ya ujumbe wa umoja wa mataifa nchini Syria ambao umeingia katika mzozano. Uingereza, Marekani, Ufaransa, Ujerumani na Ureno zinataka azimio ambalo litaweka muda wa siku kumi kwa Assad kusitisha mashambulizi yake ama akabiliwe na vikwazo chini ya ibara ya 7 ya mkataba wa umoja wa mataifa.
Urusi inakataa madai ya mataifa ya magharibi ya vikwazo.
