WATU wawili wamefariki dunia
papo hapo na wengine 15 kujeluhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kupinduka
huko Chiwanda balabala ya Tunduma- Sumbawanga.
Akizungumzi tukio hilo kamanda wa polisi
mkoani hapa Diwani Athumani
amesema kuwa tukio hilo
limetokea jana majia ya saa 11: 00 jioni
na kutaja namba za usajili wa gari hilo kuwa ni T 289 ACB, T133 aina ya
scania mali ya kampuni ya pepsi.
Pia kamanda Athumani
ameongeza kuwa gari hilo lilikuwa linatoka Mbeya
na kuelekea Sumbawanga likiwa limebebea soda huku dereva wa gali hilo aliyefahamika kwa
jina moja la Masud alikimbia baada ya ajali hiyo kutokea.
Aidha kamanda Athumani
amesema kuwa waliofariki hawajafahamika majina yao
huku miili yao
ikiwa imehidhiwa katika kituo cha afya Ndalambwa na majeruhi wanaendelea na
matibabu kituoni hapo.
