WAKAZI wa eneo la Rumbila kata ya Iwambi wameuomba uongozi wa kata na halmashauri ya
jiji kuweza kulitafutia ufumbuzi suala mabwawa ya maji kwa kupiga dawa ya kuuwa
mbu ili kuweza kunusuru afya zao .
Akizungumza na wandishi wa Elimtaa mmoja wa wakazi katika eneo hilo Bw. Rashid
Mwakipete amesema kuwa wanapata madhara makubwa kwani mbu wengi wamezaliana
katika mabwawa hayo na hivyo kupelekea tatizo la ugonjwa wa maralia .
Kwa upande wake Diwani wa
kata hiyo Gabriel Mwamwasi amesema kuwa tatizo hili ameweza kulifikisha
katika ngazi husika pamoja na uongozi wa
idara ya maji safi na maji taka mkoani hapa
na uongozi umefika mara chache na nyunyizia dawa kwa ajili ya kuuwa
vimelea vya mbu.
Hata hivyo ameongeza kuwa
uongozi umewataka wananchi wawe wavumilivu kwani muda si mrefu mabwawa hayo
yatakaushwa naytanza kutumiwa mabwawa yaliyoko katika eneo la Kalobe jijini
hapa.
Aidha Mwamwasi amesema kuwa
suala la kutupa taka katika korongo lililopo jirani na eneo la mabwawa
analipiga marufuku na kuwaasa wananchi waache mara moja ,na pia ameahidi kujitahidi kumwaga kifusi cha udongo katika eneo hilo ili liweze kufukiwa .
Joice Milambo
