Upotevu wa kijeshi na tofauti za kiitikadi zimeharakisha baadhi ya
viongozi wa al-Shabaab kujadili namna ya kuondoka katika kikundi na
kujiunga na mchakato wa kisiasa nchini Somalia na kuachana na mbinu za
vurugu za al-Shabaab, kamanda mkuu wa al-Shabaab aliiambia Sabahi.
Wakati majeshi ya AMISOM na Somalia wanaziteka kambi imara na
kushambulia kutoka pande kadhaa, wanachama wa al-Shabaab wamekubwa na
migogoro mikubwa ya ndani, makamanda huyo, ambaye hakutaka jina lake
litajwe, alisema.
Kikundi cha safu ya juu cha makamanda wa al-Shabaab hivi sasa
wanakutana katika kijiji cha Jaanale huko Shabelle ya Chini ili kuuandaa
kikundi kipya kilichojitenga kwa msaada wa baadhi ya makabila ya
Somalia, kikiwa na lengo la kuanza mazungumzo ya kisiasa na maafisa wa
serikali ya Somalia baada tarehe ya mwisho Agosti ya kumalizika kwa utawala wa mpito.
Viongozi hao wanaopinga ni pamoja na Sheikh Hassan Dahir Aweys, ambaye karibuni alitoa taarifa ya kuwalaumu viongozi wengine wa al-Shabaab kwa kumwaga damu ya Waislamu na kuua raia wasiokuwa na hatia kwa jina la Uislamu.
Wengine ni pamoja na Sheikh Mukhtar Robow Ali, anayejulikana kama Abu
Mansur; Sheikh Mohammed Ibrahim, anayejulikana kama Bilal; Sheikh
Hassan Yaqub, mdhamini wa mji wa Kismayo, ambao vikosi vya AMISOM vinasema itaanguka ndani ya wiki zijazo.
Makamanda wengine wa kanda wa al-Shabaab wanaokutana huko Jaanal ni
pamoja na: Sheikh Yusuf Isse, anayejulikana kama Kaba-kutukade na
mdhamini wa Shabelle ya Kati; Sheikh Mohammed Abdullahi Hirey,
anayejulikana kama Sheikh Mohammed Abu Abdalla, mwenye dhamana ya
Shabelle ya Chini; Sheikh Yusuf Ali Ugaas kutoka Hiran; Sheikh Ali
Mohammed Hussein, kiongozi wa zamani wa al-Shabaab mjini Mogadishu; na
Sheikh Abdifatah Mohammed Ali, muweka hazina wa zamani wa Hizbul Islam
iliyovunjika.
Makamanda kwa sasa wanamalizia msimamo rasmi wa ushirikiano huo mpya,
ambao watautangaza ndani ya wiki chache, kamanda huo wa al-Shabaab
alisema.
Alisema kuwa mkutano mwingine unaendelea huko Barawe, Shabelle ya
Chini, miongoni mwa viongozi wa al-Shabaab wenye msimao mkali zaidi.
Hawa ni pamoja na: Ahmed Abdi Godane, anayejulikana kama Sheikh Mukhtar
Abdirahman Abu al-Zubair, emir wa al-Shabaab; naibu wake, Mahad Warsame
Qaleey, anayejulikana pia kama Mahad Karateey; Sheikh Fuad Mohammed
Khalaf, anayejulikana kama Fuad Shongole, mdhamini wa ushauri na
propaganda; Sheikh Hussein Ali Fiidow, mdhamini wa sera na masuala ya
kikanda; Sheikh Ali Mahamoud Rage, anayejuliakana kama Ali Dheere,
msemaji mkuu wa kikundi; Sheikh Abdiazziz Abu Musa'ab, msemaji wa
kijeshi; and Sheikh Mohammed Hassan Omar, anayejulikana kama Mohammed
Abu Abdirahman, ambaye ni kamanda wa Mogadishu.
"Ahmed Godane amekuwa akidharau wito wa kumtaka kuachia ngazi kama
kiongozi wa kikundi, kama alivyodai kuwa emir huacha nafasi yake kwa
kufa tu, lakini hawezi kujiuzulu,au kulazimishwa kujitoa,” kamanda huyo
aliiambia Sabahi. “Hili limepelekea kuweko kwa uasi. Amri zilizotolewa
kwa viongozi wetu wawili, Mukhtar Robow na Hassan Dahir, ni kuwamaliza
baadhi ya wapiganaji wa kigeni katika kikundi wanaoshutumiwa kwa kufanya
ujasusi zilipuuzwa.”
Mwezi Aprili, ripoti ziliibuka kuwa al-Shabaab walimuua mwanajihadi aliyezaliwa Marekani Omar Hammami,
anayejulikana kama Abu Mansoor al-Amriki, kutokana na amri kutoka
Godane. Ingawaje iliripotiwa kuwa Hammami alionekana yuko hai,
al-Shabaab hawakutoa maelezo kuhusu hali yake, kitu kilichochea ripoti
za mpasuko mubwa ndani ya kikundi.
Ushirikiano wa al-Shabaab na al-Qaeda pia ulizua upinzani miongoni mwa viongozi wa al-Shabaab, kamanda alisema.
"Pia tulikataa kuwateua wageni kuwa viongozi wakuu, kuunganisha
al-Shabaab na al-Qaeda, na kuua watu wasio na hatia bila sababu yoyote
ya haki,” alisema. "Tulipinga mashambulizi ya kujitoa muhanga na
kuwalenga wananchi na wafanyakazi wa misaada.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
