MBEYA: SOKO LA SOWETO LIMA CHOO KIMOJA


WAFANYA  biashara  wa  soko  la  Soweto  wamelalamikia  uongozi  kutoridhishwa  na utendaji  wa  kazi   katika soko hilo.

Akizungumzia  suala  hilo  mmoja  wa  wafanyabiashara  sokoni  hapo aliyejitambulisha  kwa  jina  la  Ima Karoti amesema  kuwa  hali  ambayo  ipo  katika  soko  hilo  ni  mbaya  kutokana  na  kuwa  na  choo kimoja  pia  bomba moja  la  maji  ukilinganisha  na  ukubwa  wa  soko  hilo,

Kwa upande wake  mwenyekiti  wa  soko  hilo  bwana  Mbogela  amekiri kuwepo kwa matatizo  hayo  na  kusemakuwa  utendaji  wa  halmashauri  ndio    chanzo  kwani  hawatekelezi  majukum  yake kwa wakati.

Aidha  wafanyabiashara  hao  wamesema  kuwa  bomba  hilo  wakati  mwaingine  halitoi  maji  jambo  ambalo  pengine  linaweza  kuchangia  milipuko  ya  magojwa  kama  kipindupindu  na  magonjwa  mengine,

Bwana  Mbogela  amesema  kuwa  atafanya  mahojiano  na  halmashauri  ili  kuweza  kutekeleza  mambo  ambayo  yapo  kwenye  utekelezaji  yatekelezwe  kwa  wakati.