Mwanamuziki
wa R&B Chris Brown amezungumza na polisi wa jijini New York, NYPD,
kuhusiana na ugomvi uliotokea kwenye bar na uliomsababishia jereha kwenye
kidevu.
Mtandao
wa TMZ umeambiwa kuwa mwanasheria wake ameipa NYPD “ushahidi wa macho” unaodai
kuwa rapper Drake alihusika kwenye varangati hilo.
Mtandao
huo umesema umeambiwa kuwa mwanasheria wa Chris, Mark Geragos,ameenda jana NYPD
kukabidhi ushahidi unaoonesha kuwwa Drake na Meek Mill walimshambulia.
Pia umedai kuwa Drake amekuwa akishirikiana na polisi japo haujui kama ni yeye ndiye aliyeongea nao japo inaonesha kuwa wawakilishi wake ndio waliozungumza na polisi.
