NJOMBE MJI YAPATA KOCHA MPYA



BAADA ya kupata matokeo mabovu kwa muda mrefu timu ya Njombe mji imeamua kutafuta mwalimu mkuu wa timi ambaye amewasili hii leo na kuahidi matokeo ya kuwepo kwake kuanza kuonekana katika mechi ya kesho baina ya timu ya Njombe mji na Mbeya city.
Kocha Mkuu wa Njombe Mji  Ally Bushiri amesema kuwa mashabiki wa timu ya Njombe mji waanze kutaraji matokeo katika mchezo wake wa kwanza kuwa na timu hiyo na kuwa kwa michezo iliyo baki ni lazima ataifikisha timu hiyo sehemu mzuri.
Mwenyekiti wa timu hiyo Erasto Mpete amesema kuwa wakati huu mgumu ndio wa mashabiki kuonyesha kwa timu hiyo kwa kuwa matokeo inayo pitia wanataraji mabadiliko kama watakuwa na ushirikiano.
Pamoja na uongozi kuwa na matumaini hata kwa mashabiki huku kuhusu wakati wa ujio wa kocha ikiwa ni wakati wake muafaka.
Timu ya Njombe mji sasa ipo katika nafasi ya mkiani lakini bado wanamichezo mingi ambayo kama wakifanya vizuri watakuwa katika nafasi nzuri.